< Zaburi 142 >
1 Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi. Namlilia Bwana kwa sauti, nainua sauti yangu kwa Bwana anihurumie.
A Psalme of David, to give instruction, and a prayer, when he was in the cave. I cryed vnto the Lord with my voyce: with my voyce I prayed vnto the Lord.
2 Namimina malalamiko yangu mbele zake, mbele zake naeleza shida zangu.
I powred out my meditation before him, and declared mine affliction in his presence.
3 Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu, wewe ndiwe unajua njia zangu. Katika njia ninayopita watu wameniwekea mtego.
Though my spirit was in perplexitie in me, yet thou knewest my path: in the way wherein I walked, haue they priuily layde a snare for me.
4 Tazama kuume kwangu na uone, hakuna hata mmoja anayejihusisha nami. Sina kimbilio, hakuna anayejali maisha yangu.
I looked vpon my right hand, and beheld, but there was none that would knowe me: all refuge failed me, and none cared for my soule.
5 Ee Bwana, nakulilia wewe, nasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.”
Then cryed I vnto thee, O Lord, and sayde, thou art mine hope, and my portion in the land of the liuing.
6 Sikiliza kilio changu, kwa sababu mimi ni mhitaji sana; niokoe na wale wanaonifuatilia, kwa kuwa wamenizidi nguvu.
Hearken vnto my crye, for I am brought very lowe: deliuer me from my persecuters, for they are too strong for me.
7 Nifungue kutoka kifungo changu, ili niweze kulisifu jina lako. Ndipo wenye haki watanizunguka, kwa sababu ya wema wako kwangu.
Bring my soule out of prison, that I may prayse thy Name: then shall the righteous come about me, when thou art beneficiall vnto me.