< Zaburi 141 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima. Sikia sauti yangu ninapokuita.
[Psalm lal David] Nga pang nu sum, LEUM GOD. Kasreyu inge! Lipsreyu ke nga pang nu sum.
2 Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba; kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.
Eis pre luk in oana mwe kisa keng, Ac ke nga sralak pouk, eis in oana mwe kisa in eku.
3 Ee Bwana, weka mlinzi kinywani mwangu, weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.
LEUM GOD, filiya sie mwe karinginyen oalik, Ac mwe taran srungul lun ngoasrok.
4 Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya, nisije nikashiriki katika matendo maovu pamoja na watu watendao mabaya, wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.
Ikolyuwi tuh nga in tia lungse oru ma koluk, Ac in tia wi mwet koluk ke ma elos oru. Lela nga in tiana ipeis ke kufwa lalos.
5 Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. Kichwa changu hakitalikataa. Hata hivyo, maombi yangu daima ni kinyume cha watenda mabaya,
Sie mwet wo el ku in kaiyu ac aksuwosyeyu ke kulang lal, Tusruktu nga fah tia lela mwet koluk in akfulatyeyu, Mweyen nga pre in lain orekma koluk lalos pacl e nukewa.
6 watawala wao watatupwa chini kutoka kwenye majabali, waovu watajifunza kwamba maneno yangu yalikuwa kweli.
Ke mwet kol lalos sisyukla liki fulu in eot uh, Na mwet uh ac fah etu lah kas luk pwaye.
7 Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi, ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.” (Sheol h7585)
Oana sak su lipikyuki nu ke ip srisrik, Ouinge sri kaclos ac fah oan oaclik sisken kulyuk uh. (Sheol h7585)
8 Lakini nimekaza macho yangu kwako, Ee Bwana Mwenyezi, ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.
Tusruktu nga nuna lulalfongi kom, LEUM GOD Kulana. Nga suk molela lom; Nikmet lela nga in misa!
9 Niepushe na mitego waliyonitegea, kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya.
Moliyula liki mwe kwasrip su elos orala in sruokyu, Ac liki sruhf lun mwet orekma koluk.
10 Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe, wakati mimi ninapita salama.
Lela tuh mwet koluk in putatyang nu in sruhf lalos sifacna A nga fahla na siska, ac tia sruoh.

< Zaburi 141 >