< Zaburi 141 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima. Sikia sauti yangu ninapokuita.
מזמור לדוד יהוה קראתיך חושה לי האזינה קולי בקראי לך׃
2 Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba; kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.
תכון תפלתי קטרת לפניך משאת כפי מנחת ערב׃
3 Ee Bwana, weka mlinzi kinywani mwangu, weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.
שיתה יהוה שמרה לפי נצרה על דל שפתי׃
4 Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya, nisije nikashiriki katika matendo maovu pamoja na watu watendao mabaya, wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.
אל תט לבי לדבר רע להתעולל עללות ברשע את אישים פעלי און ובל אלחם במנעמיהם׃
5 Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. Kichwa changu hakitalikataa. Hata hivyo, maombi yangu daima ni kinyume cha watenda mabaya,
יהלמני צדיק חסד ויוכיחני שמן ראש אל יני ראשי כי עוד ותפלתי ברעותיהם׃
6 watawala wao watatupwa chini kutoka kwenye majabali, waovu watajifunza kwamba maneno yangu yalikuwa kweli.
נשמטו בידי סלע שפטיהם ושמעו אמרי כי נעמו׃
7 Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi, ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.” (Sheol h7585)
כמו פלח ובקע בארץ נפזרו עצמינו לפי שאול׃ (Sheol h7585)
8 Lakini nimekaza macho yangu kwako, Ee Bwana Mwenyezi, ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.
כי אליך יהוה אדני עיני בכה חסיתי אל תער נפשי׃
9 Niepushe na mitego waliyonitegea, kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya.
שמרני מידי פח יקשו לי ומקשות פעלי און׃
10 Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe, wakati mimi ninapita salama.
יפלו במכמריו רשעים יחד אנכי עד אעבור׃

< Zaburi 141 >