< Zaburi 141 >
1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima. Sikia sauti yangu ninapokuita.
Psaume de David. Éternel, je t'invoque! Accours à mon aide; Prête l'oreille à ma voix, quand je crie vers toi!
2 Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba; kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.
Que ma prière te soit agréable comme l'encens, Et mes mains tendues vers toi, comme l'oblation du soir!
3 Ee Bwana, weka mlinzi kinywani mwangu, weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.
Éternel, garde ma bouche; Veille sur mes lèvres quand elles s'ouvrent.
4 Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya, nisije nikashiriki katika matendo maovu pamoja na watu watendao mabaya, wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.
Ne permets pas que mon coeur soit entraîné au mal, Et qu'il commette des crimes avec les ouvriers d'iniquité. Que je ne prenne aucune part à leurs festins!
5 Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. Kichwa changu hakitalikataa. Hata hivyo, maombi yangu daima ni kinyume cha watenda mabaya,
Que le juste me frappe, ce sera une faveur pour moi; Qu'il me reprenne, ce sera de l'huile sur ma tête; Ma tête ne se détournera pas! Car, même en face des persécutions des méchants. Je ne fais que prier.
6 watawala wao watatupwa chini kutoka kwenye majabali, waovu watajifunza kwamba maneno yangu yalikuwa kweli.
Leurs chefs seront précipités sur les flancs des rochers! Alors on écoutera mes paroles; Car elles sont pleines de douceur.
7 Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi, ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.” (Sheol )
Comme la terre labourée et fendue par la charrue, Nos os sont dispersés à l'entrée du Sépulcre. (Sheol )
8 Lakini nimekaza macho yangu kwako, Ee Bwana Mwenyezi, ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.
C'est vers toi, Éternel, ô Seigneur, Que se tournent mes regards. Je cherche un refuge auprès de toi: N'abandonne pas mon âme!
9 Niepushe na mitego waliyonitegea, kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya.
Garde-moi du piège qu'ils m'ont tendu, Et des embûches des ouvriers d'iniquité!
10 Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe, wakati mimi ninapita salama.
Puissent les méchants tomber dans leurs propres filets, Pendant que moi, je parviendrai à m'enfuir!