< Zaburi 141 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima. Sikia sauti yangu ninapokuita.
Psaume de David. Seigneur, j'ai crié vers toi, écoute-moi; sois attentif à la voix de ma prière, quand je crie vers toi.
2 Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba; kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.
Que ma prière se dirige vers toi, comme de l'encens; que l'élévation de mes mains vers toi soit comme le sacrifice du soir.
3 Ee Bwana, weka mlinzi kinywani mwangu, weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.
Mets, Seigneur, une garde à ma bouche, et une porte de sûreté autour de mes lèvres.
4 Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya, nisije nikashiriki katika matendo maovu pamoja na watu watendao mabaya, wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.
N'incline pas mon cœur vers les paroles de la malice, pour trouver des prétextes à mes péchés, en compagnie des ouvriers d'iniquité; préserve-moi d'entrer en communication avec ceux de leur choix.
5 Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. Kichwa changu hakitalikataa. Hata hivyo, maombi yangu daima ni kinyume cha watenda mabaya,
Que le juste me réprimande avec miséricorde, et me blâme de même; mais que l'huile des pécheurs ne parfume point ma tête, que ma prière soit toujours en opposition avec leurs cupidités.
6 watawala wao watatupwa chini kutoka kwenye majabali, waovu watajifunza kwamba maneno yangu yalikuwa kweli.
Leurs puissants ont été précipités près des rochers; ils écouteront mes paroles, parce qu'elles sont adoucies.
7 Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi, ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.” (Sheol h7585)
Comme les glèbes de la terre sont brisées sur la terre, nos os ont été dispersés aux portes de l'enfer. (Sheol h7585)
8 Lakini nimekaza macho yangu kwako, Ee Bwana Mwenyezi, ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.
Seigneur, Seigneur, mes yeux sont tournés vers toi; j'ai espéré en toi; ne prends point ma vie.
9 Niepushe na mitego waliyonitegea, kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya.
Garde-moi des fils qu'on a tendus contre moi, et de la pierre de scandale des ouvriers d'iniquité.
10 Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe, wakati mimi ninapita salama.
Que les pécheurs tombent dans leurs propres filets; pour moi, je vais seul jusqu'à ce que je passe.

< Zaburi 141 >