< Zaburi 141 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima. Sikia sauti yangu ninapokuita.
Psaume de David. Yahweh, je t'invoque; hâte-toi de venir vers moi; prête l'oreille à ma voix, quand je t'invoque.
2 Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba; kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.
Que ma prière soit devant ta face comme l'encens, et l'élévation de mes mains comme l'offrande du soir!
3 Ee Bwana, weka mlinzi kinywani mwangu, weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.
Yahweh, mets une garde à ma bouche, une sentinelle à la porte de mes lèvres.
4 Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya, nisije nikashiriki katika matendo maovu pamoja na watu watendao mabaya, wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.
N'incline pas mon cœur vers des choses mauvaises; ne l'incline pas à se livrer à des actes de méchanceté avec les hommes qui commettent l'iniquité; que je ne prenne aucune part à leurs festins!
5 Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. Kichwa changu hakitalikataa. Hata hivyo, maombi yangu daima ni kinyume cha watenda mabaya,
Que le juste me frappe, c'est une faveur; qu'il me reprenne, c'est un parfum sur ma tête; ma tête ne le refusera pas, car alors je n'opposerai que ma prière à leurs mauvais desseins.
6 watawala wao watatupwa chini kutoka kwenye majabali, waovu watajifunza kwamba maneno yangu yalikuwa kweli.
Mais bientôt leurs chefs seront précipités le long des rochers; et l'on écoutera mes paroles, car elles sont agréables.
7 Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi, ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.” (Sheol h7585)
Comme lorsqu'on laboure et que l'on ameublit la terre, ainsi nos ossements sont semés au bord du schéol. (Sheol h7585)
8 Lakini nimekaza macho yangu kwako, Ee Bwana Mwenyezi, ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.
Car vers toi, Seigneur Yahweh, je tourne mes yeux; auprès de toi je cherche un refuge: n'abandonne pas mon âme!
9 Niepushe na mitego waliyonitegea, kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya.
Préserve-moi des pièges qu'ils me tendent, des embûches de ceux qui font le mal!
10 Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe, wakati mimi ninapita salama.
Que les méchants tombent dans leurs propres filets, et que j'échappe en même temps!

< Zaburi 141 >