< Zaburi 141 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima. Sikia sauti yangu ninapokuita.
A Psalm of David. LORD, I cry to thee: make haste to me; give ear to my voice, when I cry to thee.
2 Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba; kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.
Let my prayer be set forth before thee [as] incense; [and] the lifting up of my hands [as] the evening sacrifice.
3 Ee Bwana, weka mlinzi kinywani mwangu, weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.
Set a watch, O LORD, before my mouth; keep the door of my lips.
4 Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya, nisije nikashiriki katika matendo maovu pamoja na watu watendao mabaya, wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.
Incline not my heart to [any] evil thing, to practice wicked works with men that work iniquity: and let me not eat of their dainties.
5 Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. Kichwa changu hakitalikataa. Hata hivyo, maombi yangu daima ni kinyume cha watenda mabaya,
Let the righteous smite me; [it shall be] a kindness: and let him reprove me; [it shall be] an excellent oil, [which] shall not break my head: for yet my prayer also [shall be] in their calamities.
6 watawala wao watatupwa chini kutoka kwenye majabali, waovu watajifunza kwamba maneno yangu yalikuwa kweli.
When their judges are overthrown in stony places, they shall hear my words; for they are sweet.
7 Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi, ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.” (Sheol h7585)
Our bones are scattered at the grave's mouth, as when one cutteth and cleaveth [wood] upon the earth. (Sheol h7585)
8 Lakini nimekaza macho yangu kwako, Ee Bwana Mwenyezi, ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.
But my eyes [are] to thee, O GOD the LORD: in thee is my trust; leave not my soul destitute.
9 Niepushe na mitego waliyonitegea, kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya.
Keep me from the snare [which] they have laid for me, and the gins of the workers of iniquity.
10 Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe, wakati mimi ninapita salama.
Let the wicked fall into their own nets, whilst I escape.

< Zaburi 141 >