< Zaburi 141 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima. Sikia sauti yangu ninapokuita.
A psalm of David O Yahweh I call out to you make haste! to me give ear to! voice my when call I to you.
2 Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba; kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.
May it be established prayer my incense before you [the] raising of hands my an offering of evening.
3 Ee Bwana, weka mlinzi kinywani mwangu, weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.
Set! O Yahweh a guard for mouth my keep watch! over [the] door of lips my.
4 Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya, nisije nikashiriki katika matendo maovu pamoja na watu watendao mabaya, wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.
May not you turn heart my to anything - evil to practice practices - in wickedness with people [who] do wickedness and not I will eat in delicacies their.
5 Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. Kichwa changu hakitalikataa. Hata hivyo, maombi yangu daima ni kinyume cha watenda mabaya,
Let him strike me a righteous [person] - loyalty and let him rebuke me oil of head may not it refuse head my for still and prayer my [is] on evil deeds their.
6 watawala wao watatupwa chini kutoka kwenye majabali, waovu watajifunza kwamba maneno yangu yalikuwa kweli.
They have been thrown down at [the] hands of a rock judges their and they will hear words my for they are pleasant.
7 Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi, ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.” (Sheol h7585)
Like [one who] plows and [who] breaks up the earth they have been scattered bones our to [the] mouth of Sheol. (Sheol h7585)
8 Lakini nimekaza macho yangu kwako, Ee Bwana Mwenyezi, ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.
For [are] to you - (O Yahweh *L(ah+b)*) O Lord eyes my in you I take refuge may not you lay bare life my.
9 Niepushe na mitego waliyonitegea, kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya.
Keep me from [the] hands of [the] trap [which] they have laid for me and [the] snares of [those who] do wickedness.
10 Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe, wakati mimi ninapita salama.
Let them fall in own nets his wicked [people] together I until I will pass by.

< Zaburi 141 >