< Zaburi 141 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima. Sikia sauti yangu ninapokuita.
A Psalme of David. O Lord, I call vpon thee: haste thee vnto me: heare my voyce, when I cry vnto thee.
2 Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba; kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.
Let my prayer be directed in thy sight as incense, and the lifting vp of mine hands as an euening sacrifice.
3 Ee Bwana, weka mlinzi kinywani mwangu, weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.
Set a watch, O Lord, before my mouth, and keepe the doore of my lips.
4 Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya, nisije nikashiriki katika matendo maovu pamoja na watu watendao mabaya, wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.
Incline not mine heart to euill, that I should commit wicked workes with men that worke iniquitie: and let me not eate of their delicates.
5 Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. Kichwa changu hakitalikataa. Hata hivyo, maombi yangu daima ni kinyume cha watenda mabaya,
Let the righteous smite me: for that is a benefite: and let him reprooue me, and it shalbe a precious oyle, that shall not breake mine head: for within a while I shall euen pray in their miseries.
6 watawala wao watatupwa chini kutoka kwenye majabali, waovu watajifunza kwamba maneno yangu yalikuwa kweli.
When their iudges shall be cast downe in stonie places, they shall heare my wordes, for they are sweete.
7 Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi, ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.” (Sheol h7585)
Our bones lye scattered at the graues mouth, as he that heweth wood or diggeth in the earth. (Sheol h7585)
8 Lakini nimekaza macho yangu kwako, Ee Bwana Mwenyezi, ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.
But mine eyes looke vnto thee, O Lord God: in thee is my trust: leaue not my soule destitute.
9 Niepushe na mitego waliyonitegea, kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya.
Keepe me from the snare, which they haue layde for me, and from the grennes of the workers of iniquitie.
10 Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe, wakati mimi ninapita salama.
Let the wicked fall into his nettes together, whiles I escape.

< Zaburi 141 >