< Zaburi 140 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu; nilinde na watu wenye jeuri,
Müzik şefi için - Davut'un mezmuru Ya RAB, kurtar beni kötü insandan, Koru beni zorbadan.
2 ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao, na kuchochea vita siku zote.
Onlar yüreklerinde kötülük tasarlar, Savaşı sürekli körükler,
3 Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka, sumu ya nyoka iko midomoni mwao.
Yılan gibi dillerini bilerler, Engerek zehiri var dudaklarının altında. (Sela)
4 Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu; nilinde na watu wenye jeuri wanaopanga kunikwaza miguu yangu.
Ya RAB, sakın beni kötünün elinden, Koru beni zorbadan; Bana çelme takmayı tasarlıyorlar.
5 Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa, wametandaza kamba za wavu wao, wametega mitego kwenye njia yangu.
Küstahlar benim için tuzak kurdu, Haydutlar ağ gerdi; Yol kenarına kapan koydular benim için. (Sela)
6 Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.” Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia.
Sana diyorum, ya RAB: “Tanrım sensin.” Yalvarışıma kulak ver, ya RAB.
7 Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu, unikingaye kichwa changu siku ya vita:
Ey Egemen RAB, güçlü kurtarıcım, Savaş gününde başımı korudun.
8 Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao, usiache mipango yao ikafanikiwa, wasije wakajisifu.
Kötülerin dileklerini yerine getirme, ya RAB, Tasarılarını ileri götürme! Yoksa gurura kapılırlar. (Sela)
9 Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe na shida zinazosababishwa na midomo yao.
Beni kuşatanların başını, Dudaklarından dökülen fesat kaplasın.
10 Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie! Na watupwe motoni, katika mashimo ya matope, wasiinuke tena kamwe.
Kızgın korlar yağsın üzerlerine! Ateşe, dipsiz çukurlara atılsınlar, Bir daha kalkamasınlar.
11 Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi; maafa na yawawinde watu wenye jeuri.
İftiracılara ülkede hayat kalmasın, Felaket zorbaları amansızca avlasın.
12 Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki, na kuitegemeza njia ya mhitaji.
Biliyorum, RAB mazlumun davasını savunur, Yoksulları haklı çıkarır.
13 Hakika wenye haki watalisifu jina lako, na waadilifu wataishi mbele zako.
Kuşkusuz doğrular senin adına şükredecek, Dürüstler senin huzurunda oturacak.

< Zaburi 140 >