< Zaburi 140 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu; nilinde na watu wenye jeuri,
Escápame, o! Jehová, de hombre malo: de varón de iniquidades guárdame:
2 ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao, na kuchochea vita siku zote.
Que pensaron males en el corazón: cada día juntaron contiendas.
3 Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka, sumu ya nyoka iko midomoni mwao.
Aguzaron su lengua como la serpiente: veneno de áspid hay debajo de sus labios. (Selah)
4 Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu; nilinde na watu wenye jeuri wanaopanga kunikwaza miguu yangu.
Guárdame, o! Jehová, de manos de impío, de varón de injurias guárdame: que han pensado de rempujar mis pasos.
5 Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa, wametandaza kamba za wavu wao, wametega mitego kwenye njia yangu.
Soberbios me han escondido lazo y cuerdas: han tendido red: en el lugar de la senda me han puesto lazos. (Selah)
6 Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.” Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia.
He dicho a Jehová: Dios mío eres tú: escucha, o! Jehová, la voz de mis ruegos.
7 Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu, unikingaye kichwa changu siku ya vita:
Jehová, Señor, fortaleza de mi salud, cubre mi cabeza el día de las armas.
8 Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao, usiache mipango yao ikafanikiwa, wasije wakajisifu.
No des, o! Jehová, al impío sus deseos: no saques en efecto su pensamiento, y se ensoberbezcan. (Selah)
9 Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe na shida zinazosababishwa na midomo yao.
La cabeza de los que me cercan, la perversidad de sus labios la cubra.
10 Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie! Na watupwe motoni, katika mashimo ya matope, wasiinuke tena kamwe.
Caigan sobre ellos brasas: en el fuego les haga Dios caer: en profundos hoyos, de donde no salgan.
11 Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi; maafa na yawawinde watu wenye jeuri.
El varón de lengua no sea firme en la tierra: al varón de injuria cace el mal para rempujones.
12 Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki, na kuitegemeza njia ya mhitaji.
Yo sé que hará Jehová el juicio del afligido, el juicio de los menesterosos.
13 Hakika wenye haki watalisifu jina lako, na waadilifu wataishi mbele zako.
Ciertamente los justos alabarán tu nombre: los rectos estarán en tu presencia.

< Zaburi 140 >