< Zaburi 140 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu; nilinde na watu wenye jeuri,
Salmo de Davi, para o regente: Livra-me do homem mau, SENHOR; guarda-me dos homens violentos,
2 ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao, na kuchochea vita siku zote.
Que pensam maldades no coração; todo dia se reúnem para fazerem guerra.
3 Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka, sumu ya nyoka iko midomoni mwao.
Eles afiam suas línguas como a cobra; veneno de serpentes [há] debaixo de seus lábios. (Selá)
4 Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu; nilinde na watu wenye jeuri wanaopanga kunikwaza miguu yangu.
Guarda-me, SENHOR, das mãos do perverso; guarda-me do homens violentos, que pensam em empurrar os meus pés.
5 Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa, wametandaza kamba za wavu wao, wametega mitego kwenye njia yangu.
Os arrogantes me armaram ciladas e cordas; estenderam uma rede de um lado do caminho; [e] puseram laços de armadilhas para mim. (Selá)
6 Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.” Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia.
Eu disse ao SENHOR: Tu [és] meu Deus; inclina teus ouvidos à voz de minhas súplicas, SENHOR.
7 Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu, unikingaye kichwa changu siku ya vita:
Ó Senhor DEUS, força de minha salvação, cobriste minha cabeça no dia da batalha.
8 Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao, usiache mipango yao ikafanikiwa, wasije wakajisifu.
Não concedas ao perverso os desejos dele, SENHOR; não permitas suceder seu plano maligno, [pois senão] se exaltariam. (Selá)
9 Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe na shida zinazosababishwa na midomo yao.
Quanto à cabeça dos que me cercam, que a opressão de seus próprios lábios os cubra.
10 Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie! Na watupwe motoni, katika mashimo ya matope, wasiinuke tena kamwe.
Caiam sobre eles brasas vivas; faça-os cair no fogo [e] em covas profundas, [para que] não se levantem mais.
11 Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi; maafa na yawawinde watu wenye jeuri.
O homem de língua maligna não se firmará na terra; o mal perseguirá o homem violento até o derrubar.
12 Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki, na kuitegemeza njia ya mhitaji.
Eu sei que o SENHOR cumprirá a causa do aflito, o direito dos necessitados.
13 Hakika wenye haki watalisifu jina lako, na waadilifu wataishi mbele zako.
Certamente os justos agradecerão ao teu nome; os corretos habitarão perante teu rosto.

< Zaburi 140 >