< Zaburi 140 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu; nilinde na watu wenye jeuri,
Jusqu'à la Fin. Psaume de David. Seigneur, délivre-moi de l'homme pervers; arrache-moi des mains de l'homme inique.
2 ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao, na kuchochea vita siku zote.
Ceux qui n'ont eu que des pensées iniques dans le cœur, préparaient contre moi des attaques tout le jour.
3 Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka, sumu ya nyoka iko midomoni mwao.
Ils ont aiguisé leur langue comme celle du serpent; le venin de l'aspic est sous leurs lèvres.
4 Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu; nilinde na watu wenye jeuri wanaopanga kunikwaza miguu yangu.
Garde-moi, Seigneur, de la main du pécheur; arrache-moi des mains des hommes iniques. Ils se proposaient de faire trébucher mes pas:
5 Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa, wametandaza kamba za wavu wao, wametega mitego kwenye njia yangu.
Les superbes m'ont dressé des pièges cachés; et ils ont tendu des cordes, pour que mes pieds s'y prennent; sur mon chemin, ils ont mis des pierres de scandale.
6 Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.” Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia.
J'ai dit au Seigneur: tu es mon Dieu; Seigneur, prête l'oreille à la voix de ma prière.
7 Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu, unikingaye kichwa changu siku ya vita:
Seigneur, Seigneur, force de mon salut, tu as mis ma tête à l'ombre le jour du combat.
8 Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao, usiache mipango yao ikafanikiwa, wasije wakajisifu.
Seigneur, ne me livre pas au pécheur contre mon désir; ils ont eu de mauvaises pensées contre moi; ne m'abandonne point, de peur qu'ils ne soient exaltés.
9 Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe na shida zinazosababishwa na midomo yao.
Le résultat de leurs artifices, le labeur de leurs lèvres les envelopperont eux-mêmes.
10 Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie! Na watupwe motoni, katika mashimo ya matope, wasiinuke tena kamwe.
Des charbons embrasés les atteindront sur la terre; et tu les feras tomber dans les douleurs, et ils ne les pourront supporter.
11 Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi; maafa na yawawinde watu wenye jeuri.
L'homme qui parle trop ne marchera pas droit sur la terre; les calamités pourchasseront l'homme inique jusqu'à la mort.
12 Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki, na kuitegemeza njia ya mhitaji.
Je sais que le Seigneur fera justice au pauvre, et droit à l'indigent.
13 Hakika wenye haki watalisifu jina lako, na waadilifu wataishi mbele zako.
Cependant les justes rendront gloire à ton nom, et les cœurs droits habiteront avec ta face.

< Zaburi 140 >