< Zaburi 140 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu; nilinde na watu wenye jeuri,
To the Overseer. — A Psalm of David. Deliver me, O Jehovah, from an evil man, From one of violence Thou keepest me.
2 ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao, na kuchochea vita siku zote.
Who have devised evils in the heart, All the day they assemble [for] wars.
3 Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka, sumu ya nyoka iko midomoni mwao.
They sharpened their tongue as a serpent, Poison of an adder [is] under their lips. (Selah)
4 Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu; nilinde na watu wenye jeuri wanaopanga kunikwaza miguu yangu.
Preserve me, Jehovah, from the hands of the wicked, From one of violence Thou keepest me, Who have devised to overthrow my steps.
5 Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa, wametandaza kamba za wavu wao, wametega mitego kwenye njia yangu.
The proud hid a snare for me — and cords, They spread a net by the side of the path, Snares they have set for me. (Selah)
6 Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.” Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia.
I have said to Jehovah, 'My God [art] Thou, Hear, Jehovah, the voice of my supplications.'
7 Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu, unikingaye kichwa changu siku ya vita:
O Jehovah, my Lord, strength of my salvation, Thou hast covered my head in the day of armour.
8 Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao, usiache mipango yao ikafanikiwa, wasije wakajisifu.
Grant not, O Jehovah, the desires of the wicked, His wicked device bring not forth, They are high. (Selah)
9 Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe na shida zinazosababishwa na midomo yao.
The chief of my surrounders, The perverseness of their lips covereth them.
10 Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie! Na watupwe motoni, katika mashimo ya matope, wasiinuke tena kamwe.
They cause to fall on themselves burning coals, Into fire He doth cast them, Into deep pits — they arise not.
11 Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi; maafa na yawawinde watu wenye jeuri.
A talkative man is not established in the earth, One of violence — evil hunteth to overflowing.
12 Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki, na kuitegemeza njia ya mhitaji.
I have known that Jehovah doth execute The judgment of the afflicted, The judgment of the needy.
13 Hakika wenye haki watalisifu jina lako, na waadilifu wataishi mbele zako.
Only — the righteous give thanks to Thy name, The upright do dwell with Thy presence!