< Zaburi 14 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mpumbavu anasema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa; hakuna hata mmoja atendaye mema.
למנצח לדוד אמר נבל בלבו אין אלהים השחיתו התעיבו עלילה אין עשה טוב׃
2 Bwana anawachungulia wanadamu chini kutoka mbinguni aone kama wako wenye akili, wowote wanaomtafuta Mungu.
יהוה משמים השקיף על בני אדם לראות היש משכיל דרש את אלהים׃
3 Wote wamepotoka, wameharibika wote pamoja, hakuna atendaye mema. Naam, hakuna hata mmoja!
הכל סר יחדו נאלחו אין עשה טוב אין גם אחד׃
4 Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza: wale ambao huwala watu wangu kama watu walavyo mkate, hao ambao hawamwiti Bwana?
הלא ידעו כל פעלי און אכלי עמי אכלו לחם יהוה לא קראו׃
5 Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu, maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.
שם פחדו פחד כי אלהים בדור צדיק׃
6 Ninyi watenda mabaya mnakwamisha mipango ya maskini, bali Bwana ndiye kimbilio lao.
עצת עני תבישו כי יהוה מחסהו׃
7 Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni! Wakati Bwana arejeshapo wafungwa wa watu wake, Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!
מי יתן מציון ישועת ישראל בשוב יהוה שבות עמו יגל יעקב ישמח ישראל׃

< Zaburi 14 >