< Zaburi 14 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mpumbavu anasema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa; hakuna hata mmoja atendaye mema.
For the leader. Of David. Fools say in their heart, “There is no God.” Vile, hateful their life is; not one does good.
2 Bwana anawachungulia wanadamu chini kutoka mbinguni aone kama wako wenye akili, wowote wanaomtafuta Mungu.
From heaven the Lord looks out on humans, to see if any are wise, and care for God.
3 Wote wamepotoka, wameharibika wote pamoja, hakuna atendaye mema. Naam, hakuna hata mmoja!
But all have turned bad, the taint is on all; not one does good, no, not one.
4 Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza: wale ambao huwala watu wangu kama watu walavyo mkate, hao ambao hawamwiti Bwana?
Have they learned their lesson, those workers of evil? Who ate up my people, eating, devouring, never calling to the Lord.
5 Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu, maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.
Sore afraid will they be; for God is among those who are righteous,
6 Ninyi watenda mabaya mnakwamisha mipango ya maskini, bali Bwana ndiye kimbilio lao.
you may mock the plans of the poor, but the Lord is their refuge.
7 Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni! Wakati Bwana arejeshapo wafungwa wa watu wake, Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!
If only help from Zion would come for Israel! When the Lord brings his people a change of fortune, how glad will be Jacob, and Israel how joyful!

< Zaburi 14 >