< Zaburi 139 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, umenichunguza na kunijua.
Dāvida dziesma, dziedātāju vadonim. Kungs, Tu mani pārmani un pazīsti.
2 Unajua ninapoketi na ninapoinuka; unatambua mawazo yangu tokea mbali.
Tu zini manu sēdēšanu un celšanos, Tu noproti manas domas no tālienes.
3 Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu; unaelewa njia zangu zote.
Lai eju, lai guļu, Tu esi ap mani, un Tev zināmi visi mani ceļi.
4 Kabla neno halijafika katika ulimi wangu, wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.
Jo nav ne vārda uz manas mēles; redzi, Kungs, to visu Tu zini.
5 Umenizunguka nyuma na mbele; umeweka mkono wako juu yangu.
Tu meties ap mani pakaļā un priekšā un turi Savu roku pār mani.
6 Maarifa haya ni ya ajabu mno kwangu, ni ya juu sana kwangu kuyafikia.
Šī atzīšana man ir visai brīnišķa un augsta, es to nevaru izprast.
7 Niende wapi nijiepushe na Roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako?
Kur man būs aiziet no Tava Gara, un kur man būs bēgt no Tava vaiga?
8 Kama nikienda juu mbinguni, wewe uko huko; nikifanya vilindi kuwa kitanda changu, wewe uko huko. (Sheol h7585)
Ja es kāptu debesīs, tad Tu tur esi; ja es nogultos ellē, redzi, Tu tur arīdzan esi. (Sheol h7585)
9 Kama nikipanda juu ya mbawa za mapambazuko, kama nikikaa pande za mbali za bahari,
Ja es ņemtu ausekļa spārnus un paliktu jūras galā.
10 hata huko mkono wako utaniongoza, mkono wako wa kuume utanishika kwa uthabiti.
Tad arī tur Tava roka mani vadīs, un Tava labā roka mani turēs.
11 Kama nikisema, “Hakika giza litanificha na nuru inayonizunguka iwe usiku,”
Ja es sacītu: Lai tumsība mani apklāj un par nakti lai paliek gaisma ap mani:
12 hata giza halitakuwa giza kwako, usiku utangʼaa kama mchana, kwa kuwa giza ni kama nuru kwako.
Tad ir tumsība Tavā priekšā nebūtu tumša, un nakts spīdētu kā diena, tumsība būtu kā gaisma.
13 Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani; uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.
Jo Tu esi radījis manas īkstis, Tu mani esi apsedzis manas mātes miesās.
14 Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa namna ya ajabu na ya kutisha; kazi zako ni za ajabu, ninajua hayo kikamilifu.
Es Tev pateicos, ka es ļoti brīnišķi esmu darīts, brīnišķi ir Tavi darbi, un mana dvēsele to it labi zin.
15 Umbile langu halikufichika kwako, nilipoumbwa mahali pa siri. Nilipoungwa pamoja kwa ustadi katika vilindi vya nchi,
Mani kauli Tev nebija apslēpti, kad es slepenībā tapu darīts, kad es tapu iztaisīts zemes dziļumos.
16 macho yako yaliniona kabla mwili wangu haujakamilika. Siku zangu zote ulizonipangia ziliandikwa katika kitabu chako kabla haijakuwepo hata moja.
Tavas acis redzēja mani, vēl neiztaisītu pīti(miesas iedīgli), un visas nākamās dienas bija rakstītas Tavā grāmatā, kad vēl nebija nevienas.
17 Tazama jinsi yalivyo ya thamani mawazo yako kwangu, Ee Mungu! Jinsi jumla yake ilivyo kubwa!
Cik dārgas man ir Tavas domas, ak Dievs! Cik liels ir viņu skaits!
18 Kama ningezihesabu, zingekuwa nyingi kuliko mchanga. Niamkapo, bado niko pamoja nawe.
Kad tās jāskaita, tad viņu vairāk nekā smiltis. Es uzmostos un vēl esmu pie Tevis.
19 Laiti ungewachinja waovu, Ee Mungu! Ondokeni kwangu, ninyi wamwaga damu!
Ak Dievs, kaut Tu bezdievīgo nokautu, un kaut asinsvainīgie no manis atstātos.
20 Wanazungumza juu yako wakiwa na kusudi baya, adui zako wanatumia vibaya jina lako.
Tie par Tevi runā ar negantību un Tavi ienaidnieki lepojās ar viltu.
21 Ee Bwana, je, nisiwachukie wanaokuchukia? Nisiwachukie sana wanaoinuka dhidi yako?
Vai man nebūs ienīdēt, kas Tevi, Kungs, ienīst, un ieriebt, kas pret Tevi ceļas?
22 Sina kitu zaidi ya chuki dhidi yao, ninawahesabu ni adui zangu.
Ienīdēt es tos ienīstu, tie man ir ienaidnieki.
23 Ee Mungu, nichunguze, uujue moyo wangu, nijaribu na ujue mawazo yangu.
Pārbaudi mani, ak Dievs, un atzīsti manu sirdi, izmeklē mani un atzīsti manas domas,
24 Uone kama kuna njia iletayo machukizo ndani yangu, uniongoze katika njia ya milele.
Un redzi, vai es esmu negantā ceļā, un vadi mani uz mūžīgu ceļu.

< Zaburi 139 >