< Zaburi 139 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, umenichunguza na kunijua.
伶長にうたはしめたるダビデの歌 ヱホバよなんぢは我をさぐり我をしりたまへり
2 Unajua ninapoketi na ninapoinuka; unatambua mawazo yangu tokea mbali.
なんぢはわが坐るをも立をもしり 又とほくよりわが念をわきまへたまふ
3 Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu; unaelewa njia zangu zote.
なんぢはわが歩むをもわが臥をもさぐりいだし わがもろもろの途をことごとく知たまへり
4 Kabla neno halijafika katika ulimi wangu, wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.
そはわが舌に一言ありとも観よヱホバよなんぢことごとく知たまふ
5 Umenizunguka nyuma na mbele; umeweka mkono wako juu yangu.
なんぢは前より後よりわれをかこみ わが上にその手をおき給へり
6 Maarifa haya ni ya ajabu mno kwangu, ni ya juu sana kwangu kuyafikia.
かかる知識はいとくすしくして我にすぐ また高くして及ぶことあたはず
7 Niende wapi nijiepushe na Roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako?
我いづこにゆきてなんぢの聖霊をはなれんや われいづこに往てなんぢの前をのがれんや
8 Kama nikienda juu mbinguni, wewe uko huko; nikifanya vilindi kuwa kitanda changu, wewe uko huko. (Sheol h7585)
われ天にのぼるとも汝かしこにいまし われわが榻を陰府にまうくるとも 観よなんぢ彼處にいます (Sheol h7585)
9 Kama nikipanda juu ya mbawa za mapambazuko, kama nikikaa pande za mbali za bahari,
我あけぼのの翼をかりて海のはてにすむとも
10 hata huko mkono wako utaniongoza, mkono wako wa kuume utanishika kwa uthabiti.
かしこにて尚なんぢの手われをみちびき汝のみぎの手われをたもちたまはん
11 Kama nikisema, “Hakika giza litanificha na nuru inayonizunguka iwe usiku,”
暗はかならす我をおほひ 我をかこめる光は夜とならんと我いふとも
12 hata giza halitakuwa giza kwako, usiku utangʼaa kama mchana, kwa kuwa giza ni kama nuru kwako.
汝のみまへには暗ものをかくすことなく 夜もひるのごとくに輝けり なんぢにはくらきも光もことなることなし
13 Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani; uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.
汝はわがはらわたをつくり 又わがははの胎にわれを組成たまひたり
14 Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa namna ya ajabu na ya kutisha; kazi zako ni za ajabu, ninajua hayo kikamilifu.
われなんぢに感謝す われは畏るべく奇しくつくられたり なんぢの事跡はことごとくくすし わが霊魂はいとつばらに之をしれり
15 Umbile langu halikufichika kwako, nilipoumbwa mahali pa siri. Nilipoungwa pamoja kwa ustadi katika vilindi vya nchi,
われ隠れたるところにてつくられ地の底所にて妙につづりあはされしとき わが骨なんぢにかくるることなかりき
16 macho yako yaliniona kabla mwili wangu haujakamilika. Siku zangu zote ulizonipangia ziliandikwa katika kitabu chako kabla haijakuwepo hata moja.
わが體いまだ全からざるに なんぢの目ははやくより之をみ 日々かたちづくられしわが百體の一だにあらざりし時に ことごとくなんぢの冊にしるされたり
17 Tazama jinsi yalivyo ya thamani mawazo yako kwangu, Ee Mungu! Jinsi jumla yake ilivyo kubwa!
神よなんぢりもろもろの思念はわれに寶きこといかばかりぞや そのみおもひの総計はいかに多きかな
18 Kama ningezihesabu, zingekuwa nyingi kuliko mchanga. Niamkapo, bado niko pamoja nawe.
我これを算へんとすれどもそのかずは沙よりもおほし われ眼さむるときも尚なんぢとともにをる
19 Laiti ungewachinja waovu, Ee Mungu! Ondokeni kwangu, ninyi wamwaga damu!
神よなんぢはかならず惡者をころし給はん されば血をながすものよ我をはなれされ
20 Wanazungumza juu yako wakiwa na kusudi baya, adui zako wanatumia vibaya jina lako.
かれらはあしき企圖をもて汝にさからひて言ふ なんぢの仇はみだりに聖名をとなふるなり
21 Ee Bwana, je, nisiwachukie wanaokuchukia? Nisiwachukie sana wanaoinuka dhidi yako?
ヱホバよわれは汝をにくむ者をにくむにあらずや なんぢに逆ひておこりたつものを厭ふにあらずや
22 Sina kitu zaidi ya chuki dhidi yao, ninawahesabu ni adui zangu.
われ甚くかれらをにくみてわが仇とす
23 Ee Mungu, nichunguze, uujue moyo wangu, nijaribu na ujue mawazo yangu.
神よねがはくは我をさぐりてわが心をしり 我をこころみてわがもろもろの思念をしりたまへ
24 Uone kama kuna njia iletayo machukizo ndani yangu, uniongoze katika njia ya milele.
ねがはくは我によこしまなる途のありやなしやを見て われを永遠のみちに導きたまへ

< Zaburi 139 >