< Zaburi 139 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, umenichunguza na kunijua.
למנצח לדוד מזמור יהוה חקרתני ותדע׃
2 Unajua ninapoketi na ninapoinuka; unatambua mawazo yangu tokea mbali.
אתה ידעת שבתי וקומי בנתה לרעי מרחוק׃
3 Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu; unaelewa njia zangu zote.
ארחי ורבעי זרית וכל דרכי הסכנתה׃
4 Kabla neno halijafika katika ulimi wangu, wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.
כי אין מלה בלשוני הן יהוה ידעת כלה׃
5 Umenizunguka nyuma na mbele; umeweka mkono wako juu yangu.
אחור וקדם צרתני ותשת עלי כפכה׃
6 Maarifa haya ni ya ajabu mno kwangu, ni ya juu sana kwangu kuyafikia.
פלאיה דעת ממני נשגבה לא אוכל לה׃
7 Niende wapi nijiepushe na Roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako?
אנה אלך מרוחך ואנה מפניך אברח׃
8 Kama nikienda juu mbinguni, wewe uko huko; nikifanya vilindi kuwa kitanda changu, wewe uko huko. (Sheol h7585)
אם אסק שמים שם אתה ואציעה שאול הנך׃ (Sheol h7585)
9 Kama nikipanda juu ya mbawa za mapambazuko, kama nikikaa pande za mbali za bahari,
אשא כנפי שחר אשכנה באחרית ים׃
10 hata huko mkono wako utaniongoza, mkono wako wa kuume utanishika kwa uthabiti.
גם שם ידך תנחני ותאחזני ימינך׃
11 Kama nikisema, “Hakika giza litanificha na nuru inayonizunguka iwe usiku,”
ואמר אך חשך ישופני ולילה אור בעדני׃
12 hata giza halitakuwa giza kwako, usiku utangʼaa kama mchana, kwa kuwa giza ni kama nuru kwako.
גם חשך לא יחשיך ממך ולילה כיום יאיר כחשיכה כאורה׃
13 Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani; uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.
כי אתה קנית כליתי תסכני בבטן אמי׃
14 Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa namna ya ajabu na ya kutisha; kazi zako ni za ajabu, ninajua hayo kikamilifu.
אודך על כי נוראות נפליתי נפלאים מעשיך ונפשי ידעת מאד׃
15 Umbile langu halikufichika kwako, nilipoumbwa mahali pa siri. Nilipoungwa pamoja kwa ustadi katika vilindi vya nchi,
לא נכחד עצמי ממך אשר עשיתי בסתר רקמתי בתחתיות ארץ׃
16 macho yako yaliniona kabla mwili wangu haujakamilika. Siku zangu zote ulizonipangia ziliandikwa katika kitabu chako kabla haijakuwepo hata moja.
גלמי ראו עיניך ועל ספרך כלם יכתבו ימים יצרו ולא אחד בהם׃
17 Tazama jinsi yalivyo ya thamani mawazo yako kwangu, Ee Mungu! Jinsi jumla yake ilivyo kubwa!
ולי מה יקרו רעיך אל מה עצמו ראשיהם׃
18 Kama ningezihesabu, zingekuwa nyingi kuliko mchanga. Niamkapo, bado niko pamoja nawe.
אספרם מחול ירבון הקיצתי ועודי עמך׃
19 Laiti ungewachinja waovu, Ee Mungu! Ondokeni kwangu, ninyi wamwaga damu!
אם תקטל אלוה רשע ואנשי דמים סורו מני׃
20 Wanazungumza juu yako wakiwa na kusudi baya, adui zako wanatumia vibaya jina lako.
אשר יאמרך למזמה נשא לשוא עריך׃
21 Ee Bwana, je, nisiwachukie wanaokuchukia? Nisiwachukie sana wanaoinuka dhidi yako?
הלוא משנאיך יהוה אשנא ובתקוממיך אתקוטט׃
22 Sina kitu zaidi ya chuki dhidi yao, ninawahesabu ni adui zangu.
תכלית שנאה שנאתים לאויבים היו לי׃
23 Ee Mungu, nichunguze, uujue moyo wangu, nijaribu na ujue mawazo yangu.
חקרני אל ודע לבבי בחנני ודע שרעפי׃
24 Uone kama kuna njia iletayo machukizo ndani yangu, uniongoze katika njia ya milele.
וראה אם דרך עצב בי ונחני בדרך עולם׃

< Zaburi 139 >