< Zaburi 139 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, umenichunguza na kunijua.
上主,您鑒察我,也認清我:
2 Unajua ninapoketi na ninapoinuka; unatambua mawazo yangu tokea mbali.
我一舉一動,您全然認清我,您由遠處已明徹我的心思。
3 Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu; unaelewa njia zangu zote.
我或行走或躺臥,您已先知,我的一切行動,您都熟悉。
4 Kabla neno halijafika katika ulimi wangu, wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.
我的話尚未發言,上主,您已全都知曉。
5 Umenizunguka nyuma na mbele; umeweka mkono wako juu yangu.
您將我前後包圍,用您的聖手將我蔭庇。
6 Maarifa haya ni ya ajabu mno kwangu, ni ya juu sana kwangu kuyafikia.
這是超越我理智的奇事,是我不能明白的妙理。
7 Niende wapi nijiepushe na Roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako?
我往何處,才能脫離您的神能?我去那裏,才能逃避您的面容?
8 Kama nikienda juu mbinguni, wewe uko huko; nikifanya vilindi kuwa kitanda changu, wewe uko huko. (Sheol h7585)
我若上升於高天,您已在那裏,我若下降於陰府,您也在那裏。 (Sheol h7585)
9 Kama nikipanda juu ya mbawa za mapambazuko, kama nikikaa pande za mbali za bahari,
我若飛往日出的地方,我若住在海洋的西方,
10 hata huko mkono wako utaniongoza, mkono wako wa kuume utanishika kwa uthabiti.
您的雙手仍在那裏引導著我,您的聖手還在那裏扶持著我。
11 Kama nikisema, “Hakika giza litanificha na nuru inayonizunguka iwe usiku,”
我若說:願黑暗把我籠罩,光明變成黑暗將我圍包;
12 hata giza halitakuwa giza kwako, usiku utangʼaa kama mchana, kwa kuwa giza ni kama nuru kwako.
黑暗與黑夜對您並不矇矓,黑夜與白晝對您一樣光明。
13 Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani; uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.
您造成了我的五臟和六腑,您在我成胎之中締結了我。
14 Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa namna ya ajabu na ya kutisha; kazi zako ni za ajabu, ninajua hayo kikamilifu.
上主,我讚美您,因我被造驚奇神奧;您的工作千奇萬妙!我的生命,您全知曉。
15 Umbile langu halikufichika kwako, nilipoumbwa mahali pa siri. Nilipoungwa pamoja kwa ustadi katika vilindi vya nchi,
我何時在暗中構形,我何時在母胎造成,我的骨骸您全知情,
16 macho yako yaliniona kabla mwili wangu haujakamilika. Siku zangu zote ulizonipangia ziliandikwa katika kitabu chako kabla haijakuwepo hata moja.
我尚在母胎,您已親眼看見,世人的歲月尚未來到以前,都已全部記錄在冊表,都已全由您預先定好。
17 Tazama jinsi yalivyo ya thamani mawazo yako kwangu, Ee Mungu! Jinsi jumla yake ilivyo kubwa!
天主,您的策略,對我何其深奧!您策略的總數又是何其繁浩!
18 Kama ningezihesabu, zingekuwa nyingi kuliko mchanga. Niamkapo, bado niko pamoja nawe.
我若去計數,而它們多於沙粒;設若數到底,我仍同您在一起。
19 Laiti ungewachinja waovu, Ee Mungu! Ondokeni kwangu, ninyi wamwaga damu!
天主,恨不得您能殺掉惡人,叫流人血的兇遠離我身!
20 Wanazungumza juu yako wakiwa na kusudi baya, adui zako wanatumia vibaya jina lako.
他們無法無天地褻瀆您,他們不忠不義地攻擊您。
21 Ee Bwana, je, nisiwachukie wanaokuchukia? Nisiwachukie sana wanaoinuka dhidi yako?
上主,憎恨您的人,我怎能不痛惡?上主,背叛您的人,我怎能不厭惡?
22 Sina kitu zaidi ya chuki dhidi yao, ninawahesabu ni adui zangu.
我對他們深惡痛棄,視他們為我的仇敵。
23 Ee Mungu, nichunguze, uujue moyo wangu, nijaribu na ujue mawazo yangu.
天主,求您檢察我,洞知我的心曲;天主,求您考驗我,明悉我的思慮。
24 Uone kama kuna njia iletayo machukizo ndani yangu, uniongoze katika njia ya milele.
求您察看我,我是否走入岐途,求您引導我邁向上永生的道路。

< Zaburi 139 >