< Zaburi 138 >

1 Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
לדוד אודך בכל לבי נגד אלהים אזמרך׃
2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
אשתחוה אל היכל קדשך ואודה את שמך על חסדך ועל אמתך כי הגדלת על כל שמך אמרתך׃
3 Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
ביום קראתי ותענני תרהבני בנפשי עז׃
4 Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
יודוך יהוה כל מלכי ארץ כי שמעו אמרי פיך׃
5 Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
וישירו בדרכי יהוה כי גדול כבוד יהוה׃
6 Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
כי רם יהוה ושפל יראה וגבה ממרחק יידע׃
7 Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
אם אלך בקרב צרה תחיני על אף איבי תשלח ידך ותושיעני ימינך׃
8 Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.
יהוה יגמר בעדי יהוה חסדך לעולם מעשי ידיך אל תרף׃

< Zaburi 138 >