< Zaburi 138 >

1 Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
לדוד אודך בכל-לבי נגד אלהים אזמרך
2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
אשתחוה אל-היכל קדשך ואודה את-שמך-- על-חסדך ועל-אמתך כי-הגדלת על-כל-שמך אמרתך
3 Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
ביום קראתי ותענני תרהבני בנפשי עז
4 Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
יודוך יהוה כל-מלכי-ארץ כי שמעו אמרי-פיך
5 Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
וישירו בדרכי יהוה כי-גדול כבוד יהוה
6 Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
כי-רם יהוה ושפל יראה וגבה ממרחק יידע
7 Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
אם-אלך בקרב צרה-- תחיני על אף איבי תשלח ידך ותושיעני ימינך
8 Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.
יהוה יגמר בעדי יהוה חסדך לעולם מעשי ידיך אל-תרף

< Zaburi 138 >