< Zaburi 138 >

1 Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
De David. Je te célébrerai de tout mon cœur; je chanterai tes louanges devant les dieux.
2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
Je me prosternerai vers le temple de ta sainteté, et je célébrerai ton nom à cause de ta bonté et à cause de ta vérité; car tu as exalté ta parole au-dessus de tout ton nom.
3 Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
Au jour où j’ai crié, tu m’as répondu; tu as augmenté la force de mon âme.
4 Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
Tous les rois de la terre te célébreront, ô Éternel! quand ils auront entendu les paroles de ta bouche;
5 Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
Et ils chanteront dans les voies de l’Éternel, car grande est la gloire de l’Éternel.
6 Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
Car l’Éternel est haut élevé; mais il voit ceux qui sont en bas état, et il connaît de loin les hautains.
7 Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
Si je marche au milieu de la détresse, tu me feras vivre, tu étendras ta main contre la colère de mes ennemis, et ta droite me sauvera.
8 Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.
L’Éternel achèvera ce qui me concerne. Éternel! ta bonté demeure à toujours. N’abandonne pas les œuvres de tes mains.

< Zaburi 138 >