< Zaburi 138 >

1 Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
De David. Je veux te louer de tout mon cœur, te chanter sur la harpe, en présence des dieux.
2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
Je veux me prosterner dans ton saint temple, et célébrer ton nom, à cause de ta bonté et de ta fidélité, parce que tu as fait une promesse magnifique, au-dessus de toutes les gloires de ton nom.
3 Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
Le jour où je t'ai invoqué, tu m'as exaucé, tu as rendu à mon âme la force et le courage.
4 Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
Tous les rois de la terre te loueront, Yahweh, quand ils auront appris les oracles de ta bouche.
5 Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
Ils célébreront les voies de Yahweh, car la gloire de Yahweh est grande.
6 Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
Car Yahweh est élevé, et il voit les humbles, et il connaît de loin les orgueilleux.
7 Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
Si je marche en pleine détresse, tu me rends la vie, tu étends ta main pour arrêter la colère de mes ennemis, et ta droite ma sauve.
8 Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.
Yahweh achèvera ce qu'il a fait pour moi. Yahweh, ta bonté est éternelle: n'abandonne pas l'ouvrage de tes mains!

< Zaburi 138 >