< Zaburi 138 >

1 Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
to/for David to give thanks you in/on/with all heart my before God to sing you
2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
to bow to(wards) temple holiness your and to give thanks [obj] name your upon kindness your and upon truth: faithful your for to magnify upon all name your word your
3 Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
in/on/with day to call: call to and to answer me to be assertive me in/on/with soul my strength
4 Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
to give thanks you LORD all king land: country/planet for to hear: hear word lip your
5 Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
and to sing in/on/with way: conduct LORD for great: large glory LORD
6 Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
for to exalt LORD and low to see: see and high from distance to know
7 Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
if to go: walk in/on/with entrails: among distress to live me upon face: anger enemy my to send: reach hand your and to save me right your
8 Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.
LORD to cease about/through/for me LORD kindness your to/for forever: enduring deed: work hand your not to slacken

< Zaburi 138 >