< Zaburi 138 >
1 Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
David’s. I will give thee thanks with all my heart, Before the messengers of God, will I praise thee in song:
2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
I will bow down towards thy holy temple, and thank thy Name, for thy lovingkindness and for thy faithfulness, For thou hast magnified, above all thy Name, thy word!
3 Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
In the day I cried unto thee, then didst thou answer me, and didst excite me, in my soul, mightily.
4 Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
All the kings of the earth, will thank thee, O Yahweh, when they have heard the sayings of thy mouth;
5 Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
And they will sing of the ways of Yahweh, That great is the glory of Yahweh:
6 Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
Though lofty is Yahweh, yet, the lowly, he regardeth, but, the haughty—afar off, doth he acknowledge.
7 Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
Though I walk in the midst of distress, thou wilt give me life, —Because of the anger of my foes, thou wilt thrust forth thy hand, and thy right hand, will save me:
8 Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.
Yahweh, will carry through my cause, —O Yahweh! thy lovingkindness, is age-abiding, The works of thine own hands, do not thou desert.