< Zaburi 138 >
1 Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
“A psalm of David.” I will praise thee with my whole heart; Before the gods will I sing praise to thee;
2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
I will worship toward thy holy temple, And praise thy name for thy goodness and thy truth; For thy promise thou hast magnified above all thy name!
3 Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
In the day when I called, thou didst hear me; Thou didst strengthen me, and encourage my soul.
4 Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
All the kings of the earth shall praise thee, O LORD! When they hear the promises of thy mouth!
5 Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
Yea, they shall sing of the ways of the LORD; For great is the glory of the LORD.
6 Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
The LORD is high, yet he looketh upon the humble, And the proud doth he know from afar.
7 Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
Though I walk through the midst of trouble, thou wilt revive me; Thou wilt stretch forth thy hand against the wrath of my enemies; Thou wilt save me by thy right hand!
8 Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.
The LORD will perform all things for me; Thy goodness, O LORD! endureth ever: Forsake not the works of thine hands!