< Zaburi 138 >
1 Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
BY DAVID. I confess You with all my heart, I praise You before the gods.
2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
I bow myself toward Your holy temple, And I confess Your Name, For Your kindness, and for Your truth, For You have made Your saying great above all Your Name.
3 Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
In the day I called, when You answer me, You strengthen me in my soul [with] strength.
4 Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
O YHWH, all kings of earth confess You, When they have heard the sayings of Your mouth.
5 Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
And they sing in the ways of YHWH, For the glory of YHWH [is] great.
6 Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
For YHWH [is] high, and He sees the lowly, And He knows the haughty from afar.
7 Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
If I walk in the midst of distress You quicken me, You send forth Your hand against the anger of my enemies, And Your right hand saves me.
8 Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.
YHWH perfects for me, O YHWH, Your kindness [is] for all time, Do not let the works of Your hands fall!