< Zaburi 138 >
1 Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
I will praise you with my whole heart: before the gods will I sing praise to you.
2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
I will worship toward your holy temple, and praise your name for your loving kindness and for your truth: for you have magnified your word above all your name.
3 Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
In the day when I cried you answered me, and strengthened me with strength in my soul.
4 Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
All the kings of the earth shall praise you, O LORD, when they hear the words of your mouth.
5 Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
Yes, they shall sing in the ways of the LORD: for great is the glory of the LORD.
6 Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
Though the LORD be high, yet has he respect to the lowly: but the proud he knows afar off.
7 Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
Though I walk in the middle of trouble, you will revive me: you shall stretch forth your hand against the wrath of my enemies, and your right hand shall save me.
8 Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.
The LORD will perfect that which concerns me: your mercy, O LORD, endures for ever: forsake not the works of your own hands.