< Zaburi 138 >
1 Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
A Psalme of David. I will praise thee with my whole heart: euen before the gods will I praise thee.
2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
I will worship toward thine holy Temple and praise thy Name, because of thy louing kindenesse and for thy trueth: for thou hast magnified thy Name aboue all things by thy word.
3 Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
When I called, then thou heardest me, and hast encreased strength in my soule.
4 Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
All the Kings of the earth shall praise thee, O Lord: for they haue heard the wordes of thy mouth.
5 Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
And they shall sing of the wayes of the Lord, because the glory of the Lord is great.
6 Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
For the Lord is high: yet he beholdeth the lowly, but the proude he knoweth afarre off.
7 Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
Though I walke in the middes of trouble, yet wilt thou reuiue me: thou wilt stretch foorth thine hand vpon the wrath of mine enemies, and thy right hand shall saue me.
8 Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.
The Lord will performe his worke toward me: O Lord, thy mercie endureth for euer: forsake not the workes of thine handes.