< Zaburi 138 >
1 Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
Of David himself. O Lord, I will confess to you with my whole heart, for you have heard the words of my mouth. I will sing psalms to you in the sight of the Angels.
2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
I will adore before your holy temple, and I will confess your name: it is above your mercy and your truth. For you have magnified your holy name above all.
3 Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
On whatever day that I will call upon you: hear me. You will multiply virtue in my soul.
4 Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
May all the kings of the earth confess to you, O Lord. For they have heard all the words of your mouth.
5 Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
And let them sing in accordance with the ways of the Lord. For great is the glory of the Lord.
6 Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
For the Lord is exalted, and he looks with favor on the humble. But the lofty he knows from a distance.
7 Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
If I wander into the midst of tribulation, you will revive me. For you extended your hand against the wrath of my enemies. And your right hand has accomplished my salvation.
8 Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.
The Lord will provide retribution on my behalf. O Lord, your mercy is forever. Do not disdain the works of your hands.