< Zaburi 138 >
1 Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
Davidov. Zahvaljujem ti, Jahve, iz svega srca jer si čuo riječi mojih usta. Pred licem anđela pjevam tebi,
2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
bacam se nice prema svetom Hramu tvojemu. Zahvaljujem imenu tvojem za tvoju dobrotu i vjernost, jer si nada sve uzveličao obećanje svoje.
3 Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
Kad sam te zazvao, uslišio si me, dušu si moju pokrijepio.
4 Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
Nek' ti zahvaljuju, Jahve, svi kraljevi zemlje kad čuju riječi usta tvojih,
5 Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
nek' pjevaju putove Jahvine: “Zaista, velika je slava Jahvina!”
6 Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
Zaista, uzvišen je Jahve, ali gleda na ponizna, a oholicu izdaleka poznaje.
7 Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
Kroz nevolje kad budem kročio, život mi čuvaj, pruži ruku proti gnjevu mojih dušmana; nek' me tvoja spasi desnica!
8 Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.
Jahve, što ja počeh, ti dovrši! Jahve, vječna je ljubav tvoja: djelo ruku svojih ne zapusti!