< Zaburi 138 >

1 Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
上主,我要全心稱謝您,因您俯聽了我的懇祈。我要在眾神前歌頌您,
2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
朝您的聖所伏地致敬;為了您的仁慈至誠,我必要稱謝您的聖名;因為您把您的名號和您的諾言,在萬物與萬民的面前發揚彰顯,
3 Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
我幾時呼號您,您就俯允我,並將我靈魂上的力量增多。
4 Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
地上萬君聽您口的諭旨;上主,他們都必來讚頌您,
5 Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
並歌頌上主的作為說:上主的光耀偉大無比!
6 Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
上主尊高無比,仍垂顧弱小,惟對驕傲的人,卻遠遠旁眺。
7 Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
我若處於因難中,您必保全我的性命,您用右手救我,伸手拒抗仇人的憤恨。
8 Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.
上主必替我完成這工程;上主,您的仁慈永遠常存,求您不要放棄您的作品。

< Zaburi 138 >