< Zaburi 135 >

1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Deja que el Señor sea alabado. Oh siervos del Señor, alaben el nombre del Señor.
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Tú que estás en la casa del Señor, y en los espacios abiertos de la casa de nuestro Dios,
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Alaben a Jah, porque él es bueno; hagan melodía a su nombre, porque es agradable.
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
Porque el Señor tomó consigo a Jacob, y a Israel por su propiedad.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
Sé que el Señor es grande, y que nuestro Señor es más grande que todos los demás dioses.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
El Señor hizo todo lo que le agradaba, en el cielo, en la tierra, en los mares y en todas las aguas profundas.
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
Él hace que las nieblas suban desde los confines de la tierra; él hace llamas de trueno por la lluvia; Él envía los vientos desde sus almacenes.
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
El mató las primicias de Egipto, de hombres y de bestias.
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Envió señales y maravillas en medio de ti, oh Egipto, sobre Faraón y sobre todos sus siervos.
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
Él venció a las grandes naciones, y mató a los reyes fuertes;
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Sehón, rey de los amorreos, y Og, rey de Basán, y todos los reinos de Canaán;
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
Y dieron su tierra por heredad, por heredad a Israel su pueblo.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
Oh Señor, tu nombre es eterno; y el recuerdo de ti no tendrá fin.
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
Porque el Señor juzgará la causa de su pueblo; tiene compasión de sus sirvientes.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
Las imágenes de las naciones son plata y oro, obra de manos de hombres.
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
Tienen bocas, pero ninguna voz; tienen ojos, pero no ven;
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
Tienen oídos, pero no oyen; y no hay aliento en sus bocas.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Los que los hacen son como ellos; y también lo es todo el que pone su esperanza en ellos.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
Alaben a Jehová, oh hijos de Israel; alaben á Jehová, oh hijos de Aarón.
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
Alaben al Señor, hijos de Leví, alaben todos los adoradores del Señor.
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Bendito sea el Señor desde Sión, el Señor cuya casa está en Jerusalén, sea alabado Jehová.

< Zaburi 135 >