< Zaburi 135 >

1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
¡HalIelú Yah! Alabad el Nombre de Yahvé; alabadle vosotros, ciervos de Yahvé,
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
los que estáis en la casa de Yahvé, en los atrios del Templo de nuestro Dios.
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Alabad a Yah porque es un Señor bueno; cantad salmos a su Nombre, porque es suave.
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
Porque Yah se eligió a Jacob, a Israel como su bien propio.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
Porque yo sé esto: que Yahvé es grande, y que nuestro Señor es más que todas las divinidades.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
Todo cuanto Yahvé quiere lo hace en el cielo y en la tierra, en el mar y en todos los abismos.
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
Él trae las nubes desde el extremo de la tierra, hace la lluvia con los relámpagos, saca los vientos de sus depósitos.
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
Él hirió a los primogénitos de Egipto, desde el hombre hasta el ganado.
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Envió signos y prodigios a ti, oh Egipto, contra Faraón y contra todos sus vasallos.
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
Hirió a muchas naciones, y mató a reyes poderosos:
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
a Sehón, rey de los amorreos; y a Og, rey de Basan, y a todos los reyes de Canaán.
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
Y dio en herencia la tierra de ellos, en herencia a Israel, su pueblo.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
Yahvé es tu Nombre para siempre; Yahvé, tu memorial de generación en generación;
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
pues Yahvé protege a su pueblo y tiene compasión de sus siervos.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
Los ídolos de los gentiles son plata y oro, hechuras de manos de hombre:
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
tienen boca y no hablan; tienen ojos y no ven;
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
tienen orejas y no oyen, y no hay aliento en su boca.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Semejantes a ellos son quienes los hacen, quienquiera confía en ellos.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
Casa de Israel, bendecid a Yahvé; casa de Aarón, bendecid a Yahvé.
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
Casa de Leví, bendecid a Yahvé, los que adoráis a Yahvé, bendecid a Yahvé.
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Bendito sea Yahvé desde Sión, el que mora en Jerusalén.

< Zaburi 135 >