< Zaburi 135 >

1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Хвалите имя Господне, хвалите, раби Господа,
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
стоящии во храме Господни, во дворех дому Бога нашего.
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Хвалите Господа, яко благ Господь: пойте имени Его, яко добро:
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
яко Иакова избра Себе Господь, Израиля в достояние Себе:
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
яко аз познах, яко велий Господь, и Господь наш над всеми боги:
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
вся, елика восхоте Господь, сотвори на небеси и на земли, в морях и во всех безднах.
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
Возводя облаки от последних земли, молнии в дождь сотвори, изводяй ветры от сокровищ Своих.
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
Иже порази первенцы Египетския от человека до скота:
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
посла знамения и чудеса посреде тебе, Египте, на фараона и на вся рабы его.
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
Иже порази языки многи и изби цари крепки:
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Сиона царя Аморрейска и Ога царя Васанска, и вся царствия Ханаанска:
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
и даде землю их достояние, достояние Израилю людем Своим.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
Господи, имя Твое в век, и память Твоя в род и род:
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
яко судити имать Господь людем Своим, и о рабех Своих умолится.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
Идоли язык сребро и злато, дела рук человеческих:
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
уста имут, и не возглаголют: очи имут, и не узрят:
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
уши имут, и не услышат: ниже бо есть дух во устех их.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Подобни им да будут творящии я и вси надеющиися на ня.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
Доме Израилев, благословите Господа: доме Ааронь, благословите Господа: доме Левиин, благословите Господа:
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
боящиися Господа, благословите Господа.
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Благословен Господь от Сиона, живый во Иерусалиме.

< Zaburi 135 >