< Zaburi 135 >

1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Louvae ao Senhor. Louvae o nome do Senhor; louvae-o, servos do Senhor.
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Vós que assistis na casa do Senhor, nos atrios da casa do nosso Deus.
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Louvae ao Senhor, porque o Senhor é bom: cantae louvores ao seu nome, porque é agradavel.
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
Porque o Senhor escolheu para si a Jacob, e a Israel para seu proprio thesouro.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
Porque eu conheço que o Senhor é grande e que o nosso Deus está acima de todos os deuses.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
Tudo o que o Senhor quiz fez, nos céus e na terra, nos mares e em todos os abysmos.
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
Faz subir os vapores das extremidades da terra; faz os relampagos para a chuva; produz os ventos dos seus thesouros.
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
O que feriu os primogenitos do Egypto, desde os homens até ás bestas.
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
O que enviou signaes e prodigios no meio de ti, ó Egypto, contra Pharaó e contra os seus servos.
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
O que feriu muitas nações, e matou poderosos reis;
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
A Sehon, rei dos amorrheos, e a Og, rei de Basan, e a todos os reinos de Canaan.
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
E deu a sua terra em herança, em herança a Israel, seu povo.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
O teu nome, ó Senhor, dura perpetuamente; e a tua memoria, ó Senhor, de geração em geração.
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
Pois o Senhor julgará o seu povo, e se arrependerá com respeito aos seus servos.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
Os idolos das nações são prata e oiro, obra das mãos dos homens.
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
Teem bocca, mas não fallam; teem olhos, e não vêem.
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
Teem ouvidos, mas não ouvem, nem ha respiro algum nas suas boccas.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Similhantes a elles se tornem os que os fazem, e todos os que confiam n'elles.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
Casa d'Israel, bemdizei ao Senhor; casa d'Aarão bemdizei ao Senhor.
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
Casa de Levi, bemdizei ao Senhor: vós, os que temeis ao Senhor, louvae ao Senhor.
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Bemdito seja o Senhor desde Sião, que habita em Jerusalem. Louvae ao Senhor.

< Zaburi 135 >