< Zaburi 135 >
1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
KAPINA mar en Ieowa, papan Ieowa, komail kapina!
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Komail me mi nan tanpaj en Ieowa, nan pera moa en tanpaj en atail Kot.
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Kapina Ieowa, pwe Ieowa me kalanan; kauleki mar a, pwe I me mau.
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
Pwe Ieowa kotin piladar Iakop, o Ijrael, pwen japwilim a.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
Pwe i aja, Ieowa meid lapalap, o atail Kot me lapa jan kot akan karoj.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
Karoj me Ieowa kotin kupura, a kin wiada nanlan o pil ni jappa, nan madau o pajed.
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
A kin kotin wiai on tapok kan, ren dauda jan ni imwin jappa, me kin kotin wiada liol o pil katau, me kin kotin kadatala kijinian jan nan a peril kan.
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
A kotin kamelar mejeni kan nan Akipten karoj ren aramaj o man akan.
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
O kotikidan uk, Akipten, kilel o manaman akan, on Parao o na ladu kan karoj.
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
Me kotin kaloedi wein men liki kalaimun akan o kamelar nanmarki kelail akan.
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Jion, nanmarki en Amon, o Ok, nanmarki en Pajan, o wei en Kanaan karoj.
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
O kotiki on japwilim a men Ijrael jap arail, pwe ren jojoki.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
Ieowa, mar omui pan potopot eta; Main Ieowa, kataman pa omui pan jan eu kainok lel eu.
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
Pwe Ieowa pan kotin kapun japwilim a aramaj akan, o a pan kotin maki on japwilim a ladu kan.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
Dikedik en ani mal en men liki kan wiaui kida jilper o kold, me pa en aramaj wiadar.
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
Au arail mia, ap jaja lokaia, por en maj arail mia, ap jota kak kilan waja;
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
Jalon arail mia, ap jota kak ron waja, pil jota an mi nan au ar.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Me kin wiada pukat me dueta irail, o pil karoj, me kin liki irail.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
Kadaudok en Ijrael en kapina Ieowa! Kadaudok en Aron en kapina Ieowa.
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
Kadaudok en Lewi en kapina Ieowa! Komail me majak Ieowa, en kapina Ieowa!
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Kapin on Ieowa jan nan Jion, me kotikot Ierujalem! Aleluia!