< Zaburi 135 >

1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Hallelujah! Lobet den Namen Jehovahs, lobet, ihr Knechte Jehovahs!
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Ihr, die ihr steht in dem Hause Jehovahs, in den Höfen des Hauses unseres Gottes:
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Hallelujah; denn gut ist Jehovah. Singt Psalmen Seinem Namen; denn lieblich ist Er.
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
Denn Jakob hat Jah Sich erwählt, Israel zu Seinem besonderen Eigentum.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
Denn ich weiß, daß groß ist Jehovah, und unser Herr vor allen Göttern;
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
Alles, wozu Jehovah Lust hat, tut Er im Himmel und auf Erden, im Meer und allen Abgründen.
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
Er führt Dünste herauf vom Ende der Erde, macht Blitze zu Regen, bringt den Wind heraus aus Seinen Schätzen.
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
Der die Erstgeborenen Ägyptens schlug vom Menschen bis zum Vieh;
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Er sandte Zeichen und Wahrzeichen, in deine Mitte Ägypten, wider Pharao und wider alle seine Knechte.
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
Der viele Völkerschaften hat geschlagen und mächtige Könige erwürgte.
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Sichon, den König der Amoriter, und Og, den König Baschans, und alle Königreiche Kanaans.
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
Und Der ihr Land zum Erbe hat gegeben, zum Erbe Israel, Seinem Volke.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
Jehovah, Dein Name ist ewig, Jehovah, Dein Gedächtnis zu Geschlecht und Geschlecht.
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
Denn Recht wird sprechen Seinem Volk Jehovah, und es wird Ihn gereuen wegen Seiner Knechte.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
Die Götzen der Völkerschaften sind Silber und Gold, sie sind gemacht von den Händen des Menschen.
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
Einen Mund haben sie und reden nicht; Augen haben sie und sehen nicht.
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
Sie haben Ohren und nehmen nicht zu Ohren, auch ist in ihrem Mund kein Hauch.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Wie sie werden sein, die sie machen, ein jeder, der auf sie vertraut.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
O Haus Israel, segnet Jehovah; o Haus Aharons, segnet Jehovah!
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
O Haus Levi, segnet Jehovah; die ihr Jehovah fürchtet, segnet Jehovah!
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Gesegnet sei Jehovah aus Zion, Er, Der in Jerusalem wohnt. Hallelujah!

< Zaburi 135 >