< Zaburi 135 >
1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Lobet Jah! / Lobt den Namen Jahwes, / Lobt ihn, ihr Knechte Jahwes,
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Die ihr steht in Jahwes Haus, / In den Höfen des Hauses unsers Gottes!
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Lobt Jah, denn Jahwe ist gütig, / Spielt seinem Namen, denn lieblich ist er!
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
Denn Jah hat Jakob erkoren, / Israel sich zum Eigentum erwählt.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
Denn ich weiß wohl, daß Jahwe groß ist / Und unser Herr alle Götter überragt.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
Alles, was Jahwe gefiel, das hat er gemacht / Im Himmel und auf Erden, / In den Meeren und allen Tiefen.
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
Er führt Wolken herauf vom Ende der Erde, / Läßt künden durch Blitze Gewitterregen, / Holt Wind aus seinen Speichern hervor.
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
Er schlug Ägyptens Erstgeburten / Von Menschen bis zum Vieh.
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Er sandte Zeichen und Wunder / Wider dich, Ägyptenland, / Wider Pharao und all seine Knechte.
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
Er schlug viele Völker / Und tötete mächtige Könige.
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Sihon, der Amoriter König, / Und Og, den König von Basan, / Ja, machte zunichte alle Reiche Kanaans.
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
Er gab ihr Land als Erbe, / Als Erbe Israel, seinem Volk.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
Jahwe, dein Name währt ewig; / Dein Gedächtnis, Jahwe, bleibt für und für.
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
Denn Jahwe wird seinem Volk Recht schaffen / Und mit seinen Knechten Erbarmen haben.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
Der Heiden Götzen sind Silber und Gold, / Das Gebilde von Menschenhand.
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
Sie haben einen Mund und können nicht reden, / Sie haben Augen und sehen doch nicht.
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
Ohren haben sie und hören nicht, / Noch haben sie Odem in ihrem Mund.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Ihnen gleich sind, die sie bilden — / Jeder, der ihnen vertraut.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
Ihr von Israels Haus, preist Jahwe! / Ihr von Aarons Haus, preist Jahwe!
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
Ihr von Levis Haus, preist Jahwe! / Die ihr Jahwe fürchtet, preist Jahwe!
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Gepriesen sei Jahwe von Zion aus, / Er, der in Jerusalem wohnt. / Lobt Jah!