< Zaburi 135 >
1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Alleluya. Herie ye the name of the Lord; ye seruauntis of the Lord, herie ye.
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Ye that stonden in the hous of the Lord; in the hallis of `the hous of oure God.
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Herie ye the Lord, for the Lord is good; singe ye to his name, for it is swete.
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
For the Lord chees Jacob to him silf; Israel in to possessioun to him silf.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
For Y haue knowe, that the Lord is greet; and oure God bifore alle goddis.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
The Lord made alle thingis, what euere thingis he wolde, in heuene and in erthe; in the see, and in alle depthis of watris.
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
He ledde out cloudis fro the ferthest part of erthe; and made leitis in to reyn. Which bringith forth wyndis fro hise tresours;
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
which killide the firste gendrid thingis of Egipt, fro man `til to beeste.
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
He sente out signes and grete wondris, in the myddil of thee, thou Egipt; in to Farao and in to alle hise seruauntis.
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
Which smoot many folkis; and killide stronge kingis.
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Seon, the king of Ammorreis, and Og, the king of Basan; and alle the rewmes of Chanaan.
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
And he yaf the lond of hem eritage; eritage to Israel, his puple.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
Lord, thi name is with outen ende; Lord, thi memorial be in generacioun and in to generacioun.
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
For the Lord schal deme his puple; and he schal be preied in hise seruauntis.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
The symulacris of hethene men ben siluer and gold; the werkis of the hondis of men.
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
Tho han a mouth, and schulen not speke; tho han iyen, and schulen not se.
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
Tho han eeris, and schulen not here; for `nether spirit is in the mouth of tho.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Thei that maken tho, be maad lijk tho; and alle that tristen in tho.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
The hous of Israel, blesse ye the Lord; the hous of Aaron, blesse ye the Lord.
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
The hous of Leuy, blesse ye the Lord; ye that dreden the Lord, `blesse ye the Lord.
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Blessid be the Lord of Syon; that dwellith in Jerusalem.