< Zaburi 135 >

1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Praise ye the LORD. Praise ye the name of the LORD; praise [him], O ye servants of the LORD.
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Ye that stand in the house of the LORD, in the courts of the house of our God,
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Praise the LORD; for the LORD [is] good; sing praises to his name; for [it is] pleasant.
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
For the LORD hath chosen Jacob to himself, [and] Israel for his peculiar treasure.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
For I know that the LORD [is] great, and [that] our LORD [is] above all gods.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
Whatever the LORD pleased, [that] did he in heaven, and in earth, in the seas, and all deep places.
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
He causeth the vapors to ascend from the ends of the earth; he maketh lightnings for the rain; he bringeth the wind out of his treasuries.
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
Who smote the first-born of Egypt, both of man and beast.
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
[Who] sent tokens and wonders into the midst of thee, O Egypt, upon Pharaoh, and upon all his servants.
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
Who smote great nations, and slew mighty kings;
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Sihon king of the Amorites, and Og king of Bashan, and all the kingdoms of Canaan:
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
And gave their land [for] a heritage, a heritage to Israel his people.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
Thy name, O LORD, [endureth] for ever; [and] thy memorial, O LORD, throughout all generations.
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
For the LORD will judge his people, and he will repent concerning his servants.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
The idols of the heathen [are] silver and gold, the work of men's hands.
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
They have mouths, but they speak not; eyes have they, but they see not.
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
They have ears, but they hear not; neither is there [any] breath in their mouths.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
They that make them are like them: [so is] every one that trusteth in them.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
Bless the LORD, O house of Israel: bless the LORD, O house of Aaron:
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
Bless the LORD, O house of Levi: ye that fear the LORD, bless the LORD.
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Blessed be the LORD out of Zion, who dwelleth at Jerusalem. Praise ye the LORD.

< Zaburi 135 >