< Zaburi 135 >

1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Praise ye Yah, Praise ye the Name of Yahweh, Praise, O ye servants of Yahweh;
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Who stand In the house of Yahweh, In the courts of the house of our God.
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Praise ye Yah, For good is Yahweh, Sing praises to his Name, For it is full of delight;
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
For, Jacob, hath Yah chosen for himself, Israel, for his own treasure.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
For, I, know that great is Yahweh, yea, our Lord, is beyond all gods.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
Whatsoever Yahweh hath pleased, he hath done, —in the heavens and on the earth, in the seas, and all resounding deeps:
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
Causing vapours to ascend from the end of the earth, —Lightnings for the rain, hath he made, bringing forth wind out of his treasuries.
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
Who smote the firstborn of Egypt, both of man, and of beast;
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Sent signs and wonders into thy midst, O Egypt, upon Pharaoh, and upon all his servants.
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
Who smote great nations, and slew mighty kings:
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Sihon, king of the Amorites, and Og, king of Bashan, and all the kingdoms of Canaan;
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
And gave their land as an inheritance, an inheritance to Israel his people.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
O Yahweh! thy Name, is age-abiding, —O Yahweh! thy memorial, is to generation after generation.
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
For Yahweh will vindicate his people, —and, on his servants, have compassion.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
The idols of the nations, are silver and gold, the work of the hands of men:
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
A mouth, have they, but they speak not, Eyes, have they, but they see not;
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
Ears, have they, but they hear not, Nose, —there is no breath in their mouth.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Like unto them, shall be they who make them, every one who trusteth in them.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
O house of Israel! bless Yahweh, O house of Aaron! bless Yahweh;
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
O house of Levi! bless Yahweh, Ye that revere Yahweh! bless Yahweh.
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Blessed be Yahweh out of Zion, Who inhabiteth Jerusalem, Praise ye Yah!

< Zaburi 135 >