< Zaburi 135 >

1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Halleluyah ·praise Yah·! Praise Adonai’s name! Praise him, you servants of Adonai,
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
you who stand in Adonai’s house, in the courts of our God’s house.
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Halleluyah ·praise Yah·, for Adonai is good. Sing zahmar ·musical praise· to his name, for that is pleasant.
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
For Yah has chosen Jacob [Supplanter] for himself; Israel [God prevails] for his own segulah ·special treasure·.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
For I know that Adonai is great, that our Lord is above all deities.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
Whatever Adonai pleased, that he has done, in heaven and in earth, in the seas and in all deeps;
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
who causes the clouds to rise from the ends of the earth; who makes lightnings with the rain; who brings the wind out of his treasuries;
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
Who struck the firstborn of Egypt [Abode of slavery], both of man and animal;
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Who sent signs and wonders into the middle of you, Egypt [Abode of slavery], on Pharaoh, and on all his servants;
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
who struck many nations, and killed mighty kings,
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Sihon king of the Amorites [Descendants of Talkers], Og king of Bashan, and all the kingdoms of Canaan [Humbled],
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
and gave their land for a heritage, a heritage to Israel [God prevails], his people.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
Your name, Adonai, endures forever; your renown, Adonai, throughout all generations.
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
For Adonai will judge his people, and have compassion on his servants.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
The idols of the nations are silver and gold, the work of men’s hands.
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
They have mouths, but they can’t speak. They have eyes, but they can’t see.
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
They have ears, but they can’t hear; neither is there any breath in their mouths.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Those who make them will be like them; yes, everyone who trusts in them.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
House of Israel [God prevails], praise Adonai! House of Aaron [Light-bringer], praise Adonai!
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
House of Levi [United with], praise Adonai! You who fear Adonai, praise Adonai!
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Blessed be Adonai from Zion [Mountain ridge, Marking], Who dwells at Jerusalem [City of peace]. Halleluyah ·praise Yah·!

< Zaburi 135 >