< Zaburi 135 >

1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Praise ye the LORD! Praise ye the name of the LORD! Praise him, O ye servants of the LORD!
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Ye who stand in the house of the LORD, In the courts of the house of our God!
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Praise ye the LORD, for the LORD is good; Praise his name, for he is kind!
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
For the LORD chose Jacob for himself, And Israel for his own possession.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
I know that the LORD is great; That our Lord is above all gods.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
All that the LORD pleaseth, that he doeth, In heaven and upon earth, In the sea, and in all deeps.
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
He causeth the clouds to ascend from the ends of the earth; He maketh lightnings for the rain; He bringeth the wind from his store-houses.
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
He smote the first-born of Egypt, Both of man and beast.
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
He sent signs and wonders into the midst of thee, O Egypt! Against Pharaoh and all his servants!
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
He smote many nations, And slew mighty kings;
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Sihon, the king of the Amorites, And Og, the king of Bashan, And all the kings of Canaan;
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
And gave their land for an inheritance, For an inheritance to Israel, his people.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
Thy name, O LORD! endureth for ever; Thy memorial, O LORD! to all generations!
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
For the LORD judgeth his people, And hath compassion on his servants.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
The idols of the nations are silver and gold, The work of men's hands.
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
They have mouths, but they speak not; Eyes have they, but they see not.
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
They have ears, but they hear not; And there is no breath in their mouths.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
They that make them are like them; So is every one that trusteth in them.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
Praise the LORD, O house of Israel! Praise the LORD, O house of Aaron!
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
Praise the LORD, O house of Levi! Ye that fear the LORD, bless the LORD!
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Praised be the LORD out of Zion, He that dwelleth in Jerusalem! Praise ye the LORD!

< Zaburi 135 >