< Zaburi 135 >
1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Hallelujah. Praise ye the name of the Lord; praise him, O ye servants of the Lord;
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Ye that stand in the house of the Lord, in the courts of the house of our God.
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Hallelujah; for the Lord is good: sing praises unto his name; for it is lovely.
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
For Jacob hath the Lord chosen unto himself, Israel, as his peculiar treasure.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
For I well know that the Lord is great, and that our Lord is above all gods.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
Whatsoever the Lord willeth, hath he done in the heavens, and on the earth, in the seas, and in all the deeps.
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
He causeth clouds to ascend from the ends of the earth; he maketh lightnings with the rain; he bringeth forth the wind out of his treasuries.
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
[He it is] who smote the first-born of Egypt, both of man and of cattle;
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Who sent signs and wonderful tokens into the midst of thee, O Egypt, against Pharaoh, and against all his servants;
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
Who smote many nations, and slew mighty kings;
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Sichon the king of the Emorites, and 'Og the king of Bashan, and all the kingdoms of Canaan;
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
And gave their land as an inheritance, an inheritance unto Israel his people.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
O Lord, thy name [endureth] for ever: O Lord, thy memorial is throughout all generations.
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
For the Lord will espouse the cause of his people, and concerning his servants will he bethink himself.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
The idols of the nations are silver and gold, the work of the hands of men.
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
Mouths they have, but they speak not; eyes they have, but they see not;
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
Ears they have, but they hear not; neither is there any breath in their mouth.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Like them are those that make them, every one that trusteth in them.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
O house of Israel, bless ye the Lord; O house of Aaron, bless ye the Lord.
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
O house of Levi, bless ye the Lord; ye that fear the Lord, bless the Lord.
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Blessed be the Lord out of Zion, even he that resideth at Jerusalem. Hallelujah.