< Zaburi 135 >
1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Hallelujah! Praise the name of Jehovah; praise, ye servants of Jehovah,
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Ye that stand in the house of Jehovah, in the courts of the house of our God.
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Praise ye Jah; for Jehovah is good: sing psalms unto his name; for it is pleasant.
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
For Jah hath chosen Jacob unto himself, Israel for his own possession.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
For I know that Jehovah is great, and our Lord is above all gods.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
Whatsoever Jehovah pleased, he hath done in the heavens and on the earth, in the seas and all deeps;
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
Who causeth the vapours to ascend from the ends of the earth; who maketh lightnings for the rain; who bringeth the wind out of his treasuries:
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
Who smote the firstborn of Egypt, both of man and beast;
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Who sent signs and miracles into the midst of thee, O Egypt, upon Pharaoh and upon all his servants;
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
Who smote great nations, and slew mighty kings,
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Sihon king of the Amorites, and Og king of Bashan, and all the kingdoms of Canaan;
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
And gave their land for an inheritance, an inheritance unto Israel his people.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
Thy name, O Jehovah, is for ever; thy memorial, O Jehovah, from generation to generation.
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
For Jehovah will judge his people, and will repent in favour of his servants.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
The idols of the nations are silver and gold, the work of men's hands:
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
They have a mouth, and they speak not; eyes have they, and they see not;
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
They have ears, and they hear not; neither is there any breath in their mouth.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
They that make them are like unto them, — every one that confideth in them.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
House of Israel, bless ye Jehovah; house of Aaron, bless ye Jehovah;
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
House of Levi, bless ye Jehovah; ye that fear Jehovah, bless Jehovah.
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Blessed be Jehovah out of Zion, who dwelleth at Jerusalem! Hallelujah!