< Zaburi 135 >
1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Hallelujah! Praise the name of the LORD. Give praise, O servants of the LORD,
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
who stand in the house of the LORD, in the courts of the house of our God.
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Hallelujah, for the LORD is good; sing praises to His name, for it is lovely.
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
For the LORD has chosen Jacob as His own, Israel as His treasured possession.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
For I know that the LORD is great; our Lord is above all gods.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
The LORD does all that pleases Him in the heavens and on the earth, in the seas and in all their depths.
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
He causes the clouds to rise from the ends of the earth. He generates the lightning with the rain and brings forth the wind from His storehouses.
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
He struck down the firstborn of Egypt, of both man and beast.
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
He sent signs and wonders into your midst, O Egypt, against Pharaoh and all his servants.
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
He struck down many nations and slaughtered mighty kings:
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Sihon king of the Amorites, Og king of Bashan, and all the kings of Canaan.
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
He gave their land as an inheritance, as a heritage to His people Israel.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
Your name, O LORD, endures forever, Your renown, O LORD, through all generations.
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
For the LORD will vindicate His people and will have compassion on His servants.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
The idols of the nations are silver and gold, made by the hands of men.
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
They have mouths, but cannot speak; they have eyes, but cannot see;
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
they have ears, but cannot hear; nor is there breath in their mouths.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Those who make them become like them, as do all who trust in them.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
O house of Israel, bless the LORD; O house of Aaron, bless the LORD;
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
O house of Levi, bless the LORD; you who fear the LORD, bless the LORD!
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Blessed be the LORD from Zion— He who dwells in Jerusalem. Hallelujah!