< Zaburi 135 >

1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Praise the LORD! Praise the LORD’s name! Praise him, you servants of the LORD,
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
you who stand in the LORD’s house, in the courts of our God’s house.
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Praise the LORD, for the LORD is good. Sing praises to his name, for that is pleasant.
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
For the LORD has chosen Jacob for himself, Israel for his own possession.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
For I know that the LORD is great, that our Lord is above all gods.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
Whatever the LORD pleased, that he has done, in heaven and in earth, in the seas and in all deeps.
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
He causes the clouds to rise from the ends of the earth. He makes lightnings with the rain. He brings the wind out of his treasuries.
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
He struck the firstborn of Egypt, both of man and animal.
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
He sent signs and wonders into the middle of you, Egypt, on Pharaoh, and on all his servants.
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
He struck many nations, and killed mighty kings—
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Sihon king of the Amorites, Og king of Bashan, and all the kingdoms of Canaan—
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
and gave their land for a heritage, a heritage to Israel, his people.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
Your name, LORD, endures forever; your renown, LORD, throughout all generations.
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
For the LORD will judge his people and have compassion on his servants.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
The idols of the nations are silver and gold, the work of men’s hands.
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
They have mouths, but they cannot speak. They have eyes, but they cannot see.
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
They have ears, but they cannot hear, neither is there any breath in their mouths.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Those who make them will be like them, yes, everyone who trusts in them.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
House of Israel, praise the LORD! House of Aaron, praise the LORD!
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
House of Levi, praise the LORD! You who fear the LORD, praise the LORD!
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Blessed be the LORD from Zion, who dwells in Jerusalem. Praise the LORD!

< Zaburi 135 >