< Zaburi 133 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Tazama jinsi ilivyo vyema na kupendeza wakati ndugu wanapoishi pamoja katika umoja!
“A psalm of the steps, or the goings up. By David.” Behold, how good and pleasant it is For brethren to dwell together in unity!
2 Ni kama mafuta ya thamani yaliyomiminwa kichwani, yakitiririka kwenye ndevu, yakitiririka kwenye ndevu za Aroni, mpaka kwenye upindo wa mavazi yake.
It is like precious perfume upon the head, Which ran down upon the beard, The beard of Aaron; Which went down to the very border of his garments;
3 Ni kama vile umande wa Hermoni unavyoanguka juu ya Mlima Sayuni. Kwa maana huko ndiko Bwana alikoamuru baraka yake, naam, hata uzima milele.
Like the dew of Hermon, Like that which descendeth upon the mountains of Zion. For there the LORD commandeth a blessing, Even life for evermore.

< Zaburi 133 >